Hizi hapa, taarifa mpya na muhimu kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania

DIPLOMA GPA 2.9-2.0 JIUNGENI FOUNDATION PROGRAMU YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA

Kama wewe una Diploma na GPA yako ni 2.9-2.0 jiunge Foundation ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kisha utajiunga Shahada mara utakapohitimu foundation.
Kumbuka, ili uweze kujiunga foundation, wewe mwenye Diploma unapaswa kuwa na Award Verification Number (ANV) inayotolewa na NACTVET. Ikiwa huna AVN huwezi kuchaguliwa kwani sifa zitakuwa hazijatimia.

Tuma maombi yako sasa hivi kupitia www.out.ac.tz ambapo masomo yanatarajiwa kuanza mwezi Novemba 2023 na kukamilika mwezi Juni 2024.
Kama una swali usisite kuandika ujumbe kupitia nambari 0719017254. Au fika tawi la karibu la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania utahudumiwa.

FORM SIX WENYE SIFA ZIFUATAZO JIUNGENI FOUNDATION PROGRAM 

Kama wewe ni mhitimu wa Kidato cha Sita umepata DEE, EEE, CSS, EDS, ESS, DSS, EES, EEF, DEF, kwa ufupi, kama huna D mbili kwenye masomo yako lakini una pass moja na subsidiary moja jiunge Foundation Program ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambayo ni programu ya maandalizi ya kujiunga Degree katika vyuo vikuu mbalimbali.
Tuma maombi yako kupitia www.out.ac.tz

Masomo yataanza Novemba 2023 na kukamilika Juni 2024. Tuma maombi yako sasa hivi. Ada ya programu nzima ni 690,000/= ambayo hulipwa kwa awamu.

Kwa maswali niandikie sms kupitia 0719017254 nitakupatia majibu.

WENU

Dkt. Mohamed Maguo
Mhadhiri Mwandamizi na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Chuo Kikuu Huria cha Tanzania

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news