Rais Dkt.Samia ashiriki Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Doto Biteko pamoja na viongozi wengine wa Serikali wakati akipokea Maandamano ya Vijana wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Doto Biteko pamoja na viongozi wengine wa Serikali wakati akiangalia Vijana wa Halaiki walipokuwa wakionesha maumbo mbalimbali uwanjani wakati wa Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Viongozi mbalimbali pamoja wa Vyama vya Siasa wakiwa kwenye Sherehe za mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama wakati wa Heshima ya Wimbo wa Taifa wa Tanzania na ule wa Afrika Mashariki mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivalishwa Skafu na Kijana wa Skauti mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Babati kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Vijana wa Halaiki wakionesha maumbo mbalimbali wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Wakuu wa Mikoa pamoja na viongozi wengine wakiwa kwenye Sherehe za mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa Mbio hizo Abdallah Shaibu Kaimu wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha mbio hizo katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Babati Mkoani Manyara tarehe 14 Oktoba, 2023.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news