Benki Kuu yapongezwa usimamizi thabiti wa sekta ya fedha

ARUSHA-Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ameipongeza Benki Kuu ya Tanzania kwa usimamizi thabiti wa sekta ya fedha nchini pamoja na jitihada inazofanya katika kutoa elimu kwa umma kuhusu huduma za fedha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) akipewa maelezo na Naibu Gavana, Bi. Sauda Kassim Msemo, alipotembelea banda la BoT kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo alipotembea banda la BoT kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ambapo alipokelewa na Naibu Gavana, Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Bi. Sauda Kassim Msemo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) akikabidhiwa zawadi na Naibu Gavana, Bi. Sauda Kassim Msemo, alipotembelea banda la BoT kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Katikati ni Waziri wa Fedha, Dkt, Mwigulu Nchemba.

Bi. Msemo alisema kuwa katika maadhimisho hayo BoT inatoa elimu kwa umma kuhusu haki zao kutoka kwa taasisi za fedha pamoja na wajibu wa wananchi katika kutumia huduma za fedha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) akielezea jambo kwa Meneja Msaidizi Idara ya Mawasiliano, Bi. Noves Moses, alipotembelea banda la BoT kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) akipewa maelezo na Meneja Msaidizi Idara ya Mawasiliano, Bi. Noves Moses, alipotembelea banda la BoT kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Katika banda la Benki Kuu wananchi wanapata fursa yakujifunza kuhusu sera za uchumi na fedha; uwekezaji katika dhamana za serikali; usimamizi wa fedha binafsi, akiba, mkopo;namna BoT inawalinda watumiaji wa huduma za fedha; utunzaji sahihi wa noti na utambuzi wa alama za usalama; mifumo ya malipo ya taifa na namna Bodi ya Bima ya Amana inavyokinga amana za wateja wa benki na taasisi za fedha.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news