Njooni Furahika Education College kuongeza ujuzi-David Msuya

DAR ES SALAAM-Chuo cha Maendeleo ya Ujuzi, Ufundi na Viwanda (Furahika Education College) kilichopo Buguruni Malapa jijini Dar es Salaam kimeendelea kuwakaribisha wanafunzi kusoma ili kuongeza ujuzi.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa chuo hicho, David Msuya huku akisema kozi zinazolewa kwa ngazi ya Diploma ni Engineering of Computer kwa mwaka 1 na 2, ramani za majengo ndani ya mwaka 1 na 2.

Pia, kuna kozi ya Social Work mwaka 1 na 2, Airticketing, huduma ya ndani ya ndege na air hostess diploma kwa miaka miwili,ualimu na malezi diploma miaka miwili na Hotel Management miaka miwili.

"Tumekuwa tukitoa elimu ujuzi lengo ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hasan kuhusu elimu.

"Hivyo mashirika na watu mbalimbali wanakaribishwa kuleta wanafunzi na taasisi au mashirika yenye namna ya kusaidia taasisi yetu wanakaribishwa pia, ili kuwanuia watoto wa kike kupata elimu iliyo bora,"amesema Msuya. 
 
Amesema, usajili unaanza leo Novemba 7, 2023 mpaka Desemba 1, 2023 ndiyo dirisha la usajili linafungwa kwa masomo ya jioni na asubuhi. Unaweza kujiunga na masomo kupitia www.furahika.or.tz

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news