GF Vehicle Assemblers yatwaa Tuzo ya Rais

DAR ES SALAAM-Kampuni ya Unganishaji wa wa Magari nchini Tanzania GF Vehicle Assemblers iliyopo Kibaha Pwani, leo imeweza kuibuka kinara katika Tuzo ya Muunganishaji bora wa Mwaka kwenye usiku wa Tuzo za Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania wazailishaji wa ndani.
Tuzo hizo umuhimu ambazo utolewa kwa mwaka mara moja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuratibiwa na shirikisho la Viwanda nchini CTi .

Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ameweza kukabidhi Tuzo hiyo kwa Mkurugenzi wa Biashara na Masoko GF Truck Salman Karmal.
Akizungumza mara baada ya kupokea Tuzo hiyo Bw Salman Karmal amesema amesema Tuzo hiyo inawapa nguvu ya kuendelea kuzalisha( Kuunganisha Magari) kwa bora na kuongeza uzalishaji.

"Kwa mwaka 2023 tumeweza Kuzalisha gari 2000 na mategemeo yetu ni kuzalisha zaidi kwa mwaka 2024 kufikia gari 3500 kwa kuzingatia ubora na mahitaji ya soko," amesema Karmal.
Amemaliza kwa kusema GF inaendelea kuishika mkono Serikali katika sera ya wazalishaji wa ndani (local Content).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news