Haya hapa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza mwaka 2024

NA DIRAMAKINI

LEO Desemba 17, 2023 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa akiwa jijini Mwanza ametangaza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza 2024.Waziri akitangaza bofya hapa

Waziri Mchengerwa amesema, wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika Shule za Serikali kutwa na bweni hakuna atakayekosa nafasi, kwani Serikali imetenga shilingi bilioni 140.5.

Ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mapya sambamba na ukarabati wa madarasa yaliyopo kuelekea muhula mpya wa masomo utakaoanza Januari 08, 2024. “Uchaguzi ulihusisha wanafunzi 1,092,984 wakiwemo wasichana 507,933 na wavulana 585, 051 ambao walifaulu mtihani wa kuhitimu Elimu ya Msingi mwaka 2023.” amesema waziri huyo. Amesema, vigezo vilivyotumika kuchagua wanafunzi hao ni kwa kuangalia waliopata alama za ufaulu kati ya 121 hadi 300, miongoni mwao hakuna asiyepangiwa shule. “Idadi ya wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2024 imeongezeka kwa wanafunzi 16,947 sawa na ongezeko la asilimia 1.57 ikilinganishwa na wanafunzi 1,076,037 waliopata alama za kuwawezesha kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023,"amesema Mchengerwa. Amesema, miongoni mwa waliofaulu na kupangiwa kujiunga na Kidato cha Kwanza Januari, 2024 wamo wanafunzi wenye mahitaji maalum 3,587 ambapo wasichana 1,590 na wavuala 1,997.

Mheshimiwa Mchengerwa ametangaza uchaguzi huu kulingana na matokeo yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani (NECTA) hivi karibuni;

OFISI YA RAIS - TAMISEMI

UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024


BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA


CHAGUA MKOA ULIKOSOMA


ARUSHADAR ES SALAAMDODOMA
GEITAIRINGAKAGERA
KATAVIKIGOMAKILIMANJARO
LINDIMANYARAMARA
MBEYAMOROGOROMTWARA
MWANZANJOMBEPWANI
RUKWARUVUMASHINYANGA
SIMIYUSINGIDASONGWE
TABORATANGA

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news