SACP Ng’anzi awaonya madereva huku akitoa wito kwa abiria

RUVUMA-Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi,SACP Ramadhani Ng’anzi amewataka abiria wanaosafiri ndani na nje ya Mkoa Ruvuma kutoa taarifa za baadhi ya madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarini.
SACP Ng’anzi ameyasema hayo alipotembelea Kituo Kikuu cha Mabasi kilichopo eneo la Shule ya Tanga ndani ya Manispaa ya Songea Mkoa wa Ruvuma.

Amesema kuwa, huo ni mwendelezo wa ziara yake ya ukaguzi wa vyombo vya moto mkoani humo.

Pia,SACP Ng’anzi amewaonya madereva wenye tabia ya ulevi pamoja na kuendesha magari kwa mwendo kasi na watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo ya kunyang’anywa leseni zao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news