TBA yaanza kuwaondoa wadaiwa sugu

DAR ES SALAAM-Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Udalali ya Mahakama imeanza zoezi la kuwaondoka kwenye nyumba zake wapangaji wadaiwa sugu ambao ni Watumishi wa umma na viongozi wa Serikali.
Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Dar es Salaam,Arch. Bernard Mayemba amesema wameanza kuondoa wapangaji wa nyumba za XNMC zilizopo Mbezi Beach.

Ameeleza kuwa zoezi hilo, lilipaswa kuanza rasmi nchi mzima Desemba 1, 2023, lakini kwa Mkoa wa Dar es Salaam wameamua kuanza Novemba 29,mwaka huu na hakuna cha kusubiri kwani notisi imeshaisha muda wake.

“Mkoa wa Dar es Salaam una jumla ya Nyumba 1200 za watumishi wa umma waliopangisha, na kiasi kinachodaiwa kutoka kwa wapangaji ni shilingi bilioni 1.1,” amesema Arch. Mayemba.

Amesema kuwa,zoezi hilo litafanyika kwa takribani wiki tatu na kuwa hawataangalia sura ya mtu na kwamba fedha watakazopata kupitia madeni hayo yatawasaidia kukarabati nyumba na miundombinu mingine ili kuhakikisha kunakuwa na mazingira mazuri kwa wapangaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news