Chuo Kikuu Mzumbe kuwainua vijana na wajasiriamali wadogo kwa kuwapatia mitaji kwa njia ya mtandao

ARUSHA-Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa William Mwegoha amesema tafiti mbalimbali zinazofanywa na wanataaluma wa chuo hicho zimelenga kuwainua vijana wa kitanzania kwa kuwapatia mitaji kupitia uchangiaji wa umati.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya hafla ya ufunguzi.

Profesa Mwegoha amesema hayo Januari 24, 2023 wakati wa uzinduzi wa kongamano la Kimataifa linalofadhiliwa na Serikali ya Denmark kupitia mpango wa kutumia michango ya umati kwenye kuwezesha wajasiriamali wadogo nchini Tanzania (C4YET ) lililofanyika jijini Arusha.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha akihutubia katika kongamano la Kimataifa linalofadhiliwa na Serikali ya Denmark kupitia mpango wa kutumia michango ya umati kwenye kuwezesha wajasiriamali wadogo nchini Tanzania (C4YET) lililofanyika jijini Arusha.

Amesema tafiti hizo zimelenga kuangalia mbinu mbalimbali, faida kwa mlengwa na faida kwa mchangiaji ili kuwainua vijana na wajasiriamali wadogo wadogo kupitia uchangiaji wa umati.
Washiriki wa kongamano la Kimataifa la kupitia mpango wa kutumia michango ya umati kwenye kuwezesha wajasiriamali wadogo nchini Tanzania (C4YET) wakimsikiliza mgeni rasmi katika hafla ya ufunguzi, kongamono hilo la siku mbili limefanyika jijini Arusha.

“Kwa chuo chetu Mzumbe ni utafiti wenye manufaa makubwa kwasababu unachangia sana kwenye dhana ya Serikali ya kuhakikisha wajasiriamali wadogo wanawezeshwa mitaji,” amesema Prof. Mwegoha.

Amesema, kupitia kongamano hilo linalowakutanisha watalaamu kutoka vyuo mbalimbali ikiwemo Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo cha Copenhagen kutoka Denmark, watafiti watabadilishana matokeo ya utafiti na kupata njia sahihi yakutekeleza dhana ya uchangiaji wa umati.
Washiriki wa kongamano la Kimataifa la kupitia mpango wa kutumia michango ya umati kwenye kuwezesha wajasiriamali wadogo nchini Tanzania (C4YET) wakimsikiliza mgeni rasmi katika hafla ya ufunguzi, kongamono hilo la siku mbili limefanyika jijini Arusha.

Profesa Mwegoha amesema, mradi huo ulianza mwaka 2019 na ni wa miaka mitano ambao umewanufaisha vijana wa maeneo yote ya mijini na vijijini.

Naye Mratibu wa mradi huo,Dkt. Nsubili Isaga kutoka skuli ya biashara Chuo Kikuu Mzumbe amesema mradi huo umewainua wajasiriamali kutokana na kubuni nyenzo walizotumia za uandishi wa andiko lililowavutia wafadhili kwaajili ya wanataaluma kusaidia tafiti na hatimaye chuo hicho kushirikisha SIDO kwaajili ya kuwakwamua wajasiriamali vijana kwenye mikoa mitano ambayo ni Arusha, Mwanza, Dar es Salaam, Morogoro na Mbeya.
Mratibu wa Mradi wa C4YET na Mhadhiri Mwandamizi wa Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu Mzumbe Dkt. Nsubili Isaga akitoa maelezo ya awali katika kongamano la Kimataifa la kupitia mpango wa kutumia michango ya umati kwenye kuwezesha wajasiriamali wadogo nchini Tanzania (C4YET) lililofanyika jijini Arusha.

Ameongeza kuwa, jumla ya wajasiriamali 187 walipewa mafunzo hayo ambapo wajasiriamali 100 kati yao waliweza kupata mikopo yenye riba ya asilimia 5 tu inayowawezesha wao kurejesha mikopo yao kwa wakati na baadae vijana wengine watafikiwa zaidi ili wajiunge na majukwaa ya biashara mitandaoni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news