Gavana Tutuba ateta na Balozi wa EU nchini

DAR ES SALAAM-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, amekutana na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Mhe. Christine Grau katika ofisi za Benki Kuu jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao kwa pamoja wamejadiliana masuala mbalimbali kuhusu uchumi wetu ikiwemo kuanza kwa mfumo wa utekelezaji wa sera ya fedha unaotumia riba, ukuaji wa huduma jumuishi za fedha pamoja na uboreshwaji wa mifumo ya malipo.
Katika kikao hicho, Gavana Tutuba ameuomba umoja huo kuwajengea uwezo zaidi wafanyakazi wa Benki Kuu na kubadilishana uzoefu katika masuala mbalimbali ya fedha na uchumi ili waweze kutimiza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news