Tanzania, Kenya wakubaliana yaishe zuio la ndege

DAR ES SALAAM-Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kenya (KCAA) imeondoa zuio la ndege ya mizigo ya Air Tanzania kusafirisha mizigo kutoka jijini Nairobi kwenda mataifa mengine.

Uamuzi huo umefikiwa ikiwa ni saa kadhaa baada ya Mamlaka ya Usafri wa Anga nchini Tanzania (TCAA) kutangaza nia ya kuzuia safari za ndege za abiria za Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways).

Uamuzi huo ulipangwa kuanza Januari 22, 2024 uliwekwa kando baada ya mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kenya na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukubaliana kutafuta suluhu ya mgogoro huo katika kipindi cha siku tatu. Taarifa ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Tanzania iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu, Hamza Johari imesema Kenya imeruhusu ndege ya Mizigo ya ATCL kuanza kusafirisha mizigo kutokea Nairobi kuanzia leo, Januari 16. 

Aidha,baada ya uamuzi huo, Johari amesema mamlaka nchini Tanzania zinaondoa zuio la ndege za abiria za KQ kuingia katika anga la Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news