Waziri Ummy akutana na wadau wa NHIF kujadili Kitita cha Mafao

DAR ES SALAAM-Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu amekutana na wawakilishi wa wamiliki wa vituo vya afya nchini ambao ni watoa huduma za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa lengo la kujadili Kitita cha Mafao kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Lengo ni kuwa na makubaliano ya pamoja na kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa wanachama nchini.
Waziri Ummy amekutana na watoa huduma hao wa NHIF leo Januari 4, 2024 katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya zilizopo jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho, Waziri Ummy amewataka wawakikishi hao kujadiliana na kutoa maoni yao kwa uwazi na kwa kutanguliza maslahi mapana ya Watanzania ili kuwezesha upatikanaji wa huduma za matibabu kwa wananchi bila kikwazo cha fedha.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya1 Afya Dkt. John Jingu, Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu, Mwenyekiti wa APHFTA Dkt. Egina Makwabe, Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF,Bw. Juma Muhimbi, Mfamasia Mkuu wa Serikali, Bw. Daud Msasi na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw. Bernard Konga.

Pia, wawakilishi kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) pamoja na wawakilishi kutoka Bohari ya Dawa (MSD).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news