Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb), amewataka watendaji wa Serikali na taasisi za udhibiti kuwa wawezeshaji wa biashara badala ya kufungia biashara, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kulinda mitaji na maslahi ya wananchi.
Kapinga ametoa agizo hilo Agosti 10, 2026, wakati akizindua ghala la kuhifadhia mazao la Halmashauri ya Mji wa Masasi, lililopo Kata ya Mtandi lililo gharimu takribani shilingi milioni 921.
“Ukikuta kiwanda hakina mifumo mizuri usikifungie, kisaidie kiweze kurudi kwenye ramani; ukikuta mtu hana leseni ya biashara, msaidie apate leseni badala ya kumfungia biashara.”
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo
























