GST, JOGMEC ya Japan kushirikiana katika tafiti

CAPE TOWN-Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeingia makubaliano na Serikali ya Japan kupitia Shirika lake linaloshughulikia masuala ya Madini ya Metali, Gesi na Mafuta (JOGMEC) kufanya tafiti za Miamba na Madini nchini Tanzania.
Makubaliano hayo yamefikiwa kupitia kikao kilichofanyika Februari 6, 2024 jijini Cape Town, Afrika Kusini baina ya taasisi ya GST na Shirika la JOGMEC.

Kwa upande wa Tanzania, imewakilishwa na Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa, Kamishna wa Madini, Dkt. AbdulRahman Mwanga, Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba na Mkurugenzi wa Kanzidata ya Taarifa za Madini,Bi. Hafsa Maulid.

GST inashiriki Mkutano wa Mining Indaba unaoendelea jijini Capetown, nchini Afrika Kusini ulioanza tarehe 05 Januari na unategemea kufikia tamati tarehe 08 Februari, 2024.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news