Pinda alia na ucheleweshaji Barabara ya Kibaoni-Sitalike

NA MUNIR SHEMWETA

MBUNGE wa Jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amemlilia Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa kufuatia ucheleweshaji ujenzi wa barabara ya km 70 kutoka Kibaoni- Sitalike katika halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele mkoani Katavi.
Mbunge wa Jimbo la Kavuu ambaye ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akikagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Sitalike- Kibaoni wilayani Mlele mkoani Katavi tarehe 3 Februari 2024. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI).

Barabara hiyo inayojengwa na Kampuni ya Kichina ya China Railway Seventh Gruop Co ltd ujenzi wake uliianza mwishoni mwa mwaka 2022 na kutarajiwa kukamilika mwaka huu.

Mhe Pinda alitembelea eneo la Barabara hiyo tarehe 3 Februari 2024 akiwa katika ziara ya jimboni kwake Kavuu kukagua shughuli za maendeleo pamoja na kuwajulia hali wale wananchi wa jimbo lake waliopatwa na ugonjwa wa kipindupindu.
Mbunge wa Jimbo la Kavuu ambaye ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akisisitiza jambo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Sitalike- Kibaoni wilayani Mlele mkoani Katavi tarehe 3 Februari 2024.

Kwa mujibu wa Mbunge huyo wa jimbo la Kavuu barabara hiyo ya Kibaoni- Sitalike ujenzi wake ulitakiwa uwe umefikia asilimia 50 lakini mpaka kufikia sasa ujenzi huo unasuasua.
Mbunge wa Jimbo la Kavuu na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Sitalike- Kibaoni wilayani Mlele mkoa wa Katavi kutoka kwa mkaguzi Sospeter Mahujiro alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo tarehe 3 Februari 2024.

"Barabara hii ni muhimu sana kwa wananchi wa jimbo la Kavuu na halmashauri nzima ya Mpimbwe kwa kuwa ni ya kimkakati kwa uchumi wa wana Mpimbwe,"alisema Mhe. Pinda.

Amemuaomba Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashingwa kuitupia jicho la karibu barabara hiyo kutokana na umuhimu wake lakini pia kuwaokoa wananchi wa jimbo lake la Kavuu kutokana na adha wanayoipata wanapoitumia barabara hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Kavuu ambaye ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Sitalike- Kibaoni kutoka kwa mkaguzi Sospeter Mahujiro alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo tarehe 3 Februari 2024.

Halmashauri ya Mpimbwe mkoani Katavi ni moja ya eneo la uzalishaji mazao mbalimbali ya kilimo kama vile Mpunga, mahindi, ufuta na alizeti na kukamilika kwa barabara hiyo itakuwa kichocheo kikubwa cha usafirishaji mazao hayo na kuwezesha wananchi kuinuka kiuchumi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news