Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Mei 15,2024

DAR-Ubalozi wa India nchini Tanzania umekutana na kufanya mazungumzo na Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kwa lengo la kupata taarifa zaidi kuhusu zoezi la kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia linalotarajiwa kufanyika Tanzania Bara mwaka huu.

Mazungumzo hayo yamefanyika Mei 14, 2024 katika Ofisi za PURA jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Katibu wa Pili wa Balozi wa India nchini Tanzania (Masuala ya Biashara),Bw. Narender Kumar na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Mhandisi Danstan Asanga.

Akizungumza katika kikao kati ya pande hizo, Bw. Kumar alieleza kuwa, mara baada ya kusikia mpango wa Serikali wa kunadi vitalu vya mafuta na gesi asilia kupitia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati mwaka 2024/25, Ubalozi wa India Nchini Tanzania uliona vyema kukutana na Mamlaka husika kufahamu kwa mapana kuhusu suala hilo ili waweze kutoa taarifa kamili kwa kampuni na wadau nchini India.









Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news