DAR-Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Prof. Najat Kassim Mohammed amehitimisha ziara yake ya kikazi katika ofisi za tume, Kanda ya Mashariki jijini Dar es Salaam.


Aidha, akiwa katika ziara ya Kanda ya Mashariki, Prof. Najat pia alitembelea Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) na kukutana na uongozi wa hospitali hiyo.
Pia, Mkurugenzi Mkuu alifanya kikao cha pamoja katika kuangalia maeneo ya ushirikiano yanayohusu matumizi ya teknolojia ya nyuklia na mionzi katika uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali.
