DODOMA-Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo inatarajiwa kutia saini Mkataba wa ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu jijini Dodoma Februari 13, 2025 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa uwanja huo.
Waziri Prof. Kabudi ameyasema hayo leo Februari 11, 2025 Bungeni jijini Dodoma wakati akichangia mjadala kuhusu taarifa ya kamati ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo ambapo ameeleza kuwa pesa za ujenzi huo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mkandarasi wa ujenzi huo tayari ameshapatikana.Aidha,uwanja huo utakua na uwezo wa kubeba watu 32,000 kwa wakati mmoja.