Gavana Tutuba ashiriki kikao cha Ujumbe wa Tanzania na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa IMF

WASHINGTON-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba, ameshiriki kikao kati ya ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Adran Ubisse.
Kikao hicho kililenga kujadili masuala ya kiuchumi pamoja na athari za mabadiliko ya sera za Marekani dhidi ya nchi za Afrika.

Dkt. Nchemba alieleza kuwa Tanzania imejipanga kukabiliana na athari za kusitishwa kwa misaada kutoka Marekani kwa kutegemea rasilimali za ndani kupitia Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2025/2026.
Alibainisha kuwa Serikali imejipanga kubana matumizi ya kawaida na kuelekeza fedha zaidi kwenye huduma muhimu za jamii pamoja na sekta za uzalishaji, kwa lengo la kulinda uchumi wa taifa na kuhakikisha wananchi wanaendelea kupata huduma muhimu bila kutegemea misaada ya nje.
Mazungumzo hayo yamefanyika kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya IMF na Benki ya Dunia, inayoendelea jijini Washington D.C., Marekani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news