Hii ni operesheni ya nchi na ndiyo kazi tuliyotumwa na Rais Dkt.Samia-Naibu Waziri Mwinjuma

DURBAN-Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma amesema kuwa Serikali iko bega kwa bega na vilabu vya mpira wa miguu kuhakikisha michezo nchini inapata hadhi inayostahili.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma kwenye picha ya pamoja na wachezaji wa Simba SC baada ya kufuzu kutinga fainali ya Shirikisho la Afrika (CAFCC) Aprili 27, 2025 nchini Afrika Kusini.

Mhe. Mwinjuma amesema hayo wakati akiwapongeza Simba SC baada ya kufuzu kutinga fainali ya kombe la Shirikisho la Afrika (CAFCC), Aprili 27, 2025 nchini Afrika kusini walipokuwa wakichuana na mwenyeji wake Stellenbosch.
"Tunafahamu kuwa huu mchezo una wapenzi wengi, hivyo sisi kama Serikali tunafanya kile kilicho ndani ya uwezo wetu kuhakikisha hatuwaangashi wapenzi wa soka nchini," amesema Mhe. Mwinjuma.

Aidha, Mhe. Mwinjuma amebainisha kuwa soka la Tanzania limepanda kwa kiasi kikubwa na timu hizo sasa zinafika mashindano makubwa na kupambana hadi kufikia hatua za juu zaidi.
“Mpira wetu umepanda kweli, kuna uwezekano mkubwa safari hii tukawa mabingwa wa kombe hili, tuache figisufigisu, tuombeane Mungu, hii ni kwa ajili ya Tanzania n ani Oparesheni ya nchi,” amesema Mhe. Hamis Mwinjuma.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mwinjuma amewataka Watanzania kutambua kuwa soka la mpira wa miguu nchini limepanda na kufikia hatua kubwa hivyo kusherehekea mafanikio ambayo timu zetu zinafikia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news