Papa Francis amefariki na siri ya Vatican

Na Guillaume Vld

SI watu wengi wanafahamu kwamba Vatikani ina maktaba ya chini ya ardhi, yenye urefu wa zaidi ya maili 50 (sawa na zaidi ya kilomita 80).

Katika maktaba hiyo ya ardhini, pia kuna shehena ya hifadhi ya vitu ambavyo vina siri ya historia ya ulimwengu.

Ndio, narudia kusema, maktaba ya ardhini yenye urefu wa maili 50, ambapo hii sio dhana wala habari ya nadharia; ni ukweli usiopingika.

Kumbukumbu za Siri ya Vaticani (Vatican Secret Archives), ni halisi na ziko katika mojawapo ya tovuti za Vaticani ambazo ni mahsusi kwa ajili ya masuala ya kidini na kitamaduni duniani.

Aidha, kumbukumbu hizo za jumla ya urefu wa maili 53 zimepangwa vizuri katika mashelvu yenye katalogi 35,000, zikiwemo dokumenti ambazo zina umri wa zaidi ya miaka 1,200.

Jina "Kumbukumbu za Siri" linaongeza usiri katika hizo siri zao nyingi, ambazo hujumuisha mambo ya siri za hii dunia zilizofichwa katika kile kinachoitwa Stori za Kiza (dark stories).

Kwa kuwa hizo faharasa (indexes) si za wazi kwa umma na zinaweza kupatikana tu kwa wanasayansi wa taaluma flani pekee, watu wengi wanafikiri kwamba kumbukumbu hizo zina mambo ya kushtua au hata ya ajabu.

Baadhi ya watu wanaofahamu uwepo wa siri hizo na ambao hawana uwezo wa kwenda huko ardhini kuzipekua, wanaamini kwamba huenda Vatikani inaficha ukweli kuhusu viumbe wa kigeni (aliens) kutoka anga au sayari zingine.
PICHA: Papa Francis enzi ya uhai wake, pamoja na dhana ya picha ikionyesha uwepo wa viumbe kutoka anga za mbali; na ambao wanafanyakazi na Vatikani katika maktaba yake ya ardhini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news