Serikali yaufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa

DAR-Serikali imeufunga Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam kwa muda kuanzia Aprili 9, 2025 ili kupisha marekebisho ya eneo la kuchezea (pitch) lililopata athari kubwa kufuatia mvua zilizonyesha zilizofuatiwa pia na mechi ya robo fainali Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba SC na Al Masry ya Misri.
Taarifa rasmi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeeleza kuwa,Timu ya Wataalamu itaanza mara moja kufanya tathmini ya kina ya madhara yaliyojitokeza na tarehe ya kufunguliwa kwa uwanja huo itatangazwa hapo baadae.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news