Tanzania,Saudi Arabia zakubaliana kushirikiana kuendeleza Sayansi na Elimu

RIYADH-Tanzania na Saudi Arabia zimesaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano Katika kuendeleza Sayansi na Elimu.
Hati hiyo ya Ushirikiano imesainiwa tarehe 13, Aprili, 2025, jijini Riyadh nchini Saudi Arabia kati ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya Tanzania na Wizara ya Elimu ya Saudi Arabia ikilenga kuendeleza Sayansi Teknolojia na Elimu.

Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda na Waziri wa Elimu na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya HCDP ya Saudi Arabia Mhe. Yousef bin Abdullah Al-Benyan.
Makubaliano hayo yanalenga kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia katika masuala ya elimu, utafiti na sayansi.

Tukio hilo limeshuhudiwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Dkt. Moh’d Juma Abdalla, Katibu Mkuu Wizara ya elimu Sayansi na Teknolojia Prof.Carolyne Nombo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Wakurugenzi na maafisa wengine wa Wizara ya elimu

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news