Biashara United yashuka daraja

MARA-Biashara United kutoka Musoma mkoani Mara imeshuka rasmi daraja kutoka Ligi ya Championship ya NBC mpaka First League.
Ni baada ya kucheza michezo 29 na kupata alama 15 ikifunga mabao 24 kufungwa mabao 43 na imebakiza mchezo mmoja ili kukamilisha msimu ambapo hata ikishinda haitaweza kupata alama za kuifanya kucheza play off.

Biashara United ilishuka daraja kutoka Ligi Kuu ya NBC katika msimu wa 2021/2022 ambapo ilitolewa na timu ya Azam baada ya kufungwa mabao 4-0 na kuwafanya kucheza Ligi ya Championship kwa misimu mitatu na sasa wameshuka kwenda Ligi ya First League.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news