DAR-Bodi ya Ligi Tanzania imetoa ratiba ya mechi zilizosalia kwenye NBC Premier League pamoja na CRDB Bank Federation Cup, ambapo mchezo kati ya Yanga dhidi ya Simba, sasa kupigwa Juni 15, 2025 majira ya saa 11:00 jioni katika dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Ligi hiyo inatarajiwa kumalizika Juni 22, 2025 huku fainali ya CRDB Bank Federation Cup kupigwa kati ya Juni 26 hadi 28,2025.