DCEA yatoa elimu dhidi ya madhara ya dawa za kulevya kwa wanawake wajawazito,wanaonyonyesha

RUKWA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kupitia Ofisi ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, imetoa elimu kwa akinamama wajawazito na wanaonyonyesha katika Kituo cha Afya Mazwi, Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa.
Mafunzo hayo yalilenga kuwaelimisha juu ya madhara ya matumizi ya dawa za kulevya kwa mama na mtoto, hasa wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua, sambamba na mbinu za kujenga familia salama isiyoathirika na matumizi ya dawa hizo.
Aidha, washiriki walifundishwa kuhusu malezi bora, mawasiliano kati ya mzazi na mtoto, pamoja na namna ya kuwalinda watoto dhidi ya bidhaa hatarishi zenye kemikali au dawa za kulevya kama biskuti, pipi, keki na vinywaji vinavyolenga watoto kwani baadhi ya bidhaa hizo huwalenga watoto kama soko la baadaye la dawa za kulevya, hali inayotishia ustawi wa taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news