Magazeti leo Mei 23,2025

DAR-Msanii maarufu wa filamu nchini na Mkurugenzi wa Taasisi ya Wema wa Mama, Wema Sepetu, ameomba radhi kwa kuvaa mavazi yaliyozua mjadala kuhusu maadili na kuahidi kuwa tukio hilo halitarudiwa tena.
Wema ameyasema hayo baada ya kuitikia wito wa Bodi ya Filamu Tanzania kufuatia picha zake zilizosambaa mitandaoni na kuzua mijadala mikali kuhusu maadili ya wasanii.
Akizungumza baada ya kikao hicho, Wema alisema kilikuwa si kikao rasmi cha kisheria bali ni cha mazungumzo ya kukumbushana kuhusu maadili ya wasanii nchini.

“Nilikuja Bodi ya Filamu kuitikia wito. Kikao hakikuwa rasmi, bali kilikuwa cha kukumbushana juu ya maadili. Nimeyasikia na nimeyazingatia.

“Kufanya kosa si kosa, bali kurudia kosa ndio kosa. Nachukua nafasi hii kuomba msamaha kwa wote niliowakwaza. Nimejifunza, na haitajirudia tena,” alisisitiza Wema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news