Magazeti leo Mei 24,2025

DAR-Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amezindua mradi wa awamu ya pili wa ujenzi na uendelezaji wa Kituo cha Umahiri wa Sayansi ya Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaotekelezwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).
Mradi huo unatekelezwa katika Kampasi ya Mloganzila ya MUHAS, ukigharimu dola milioni 83 kupitia mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), na unasimamiwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. kupitia mradi huu, hospitali ya kisasa ya magonjwa ya moyo na mishipa ya damu itajengwa pamoja na kuwekwa vifaa tiba vya kisasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news