Rais Daniel Chapo awasili Zanzibar kwa ziara ya kikazi

ZANZIBAR-Rais wa Msumbiji Mheshimiwa Daniel Chapo tayari amewasili Zanzibar akitokea jijini Dar Es Salaam ambapo akiwa Zanzibar atakua na ziara fupi ya kikazi.
Akiwa Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume amepokelewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Hamza Hassan Juma pamoja na viongozi wengine akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Nchini Tanzania Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo.
Rais Chapo atakutana na Mwenyeji wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi pamoja na kutembelea kituo cha Uvuvi cha Bahari kuu Fumba.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news