Rais Dkt.Mwinyi arejea Zanzibar

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewasili Zanzibar akitokea Zimbabwe, ambako alishiriki Kikao cha Wakuu wa Nchi na Viongozi wa Serikali wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kilichojadili Uhifadhi wa Hifadhi zinazovuka mipaka.
Alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Leo tarehe 24 Mei 2025 alipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Idrisa Kitwana Mustafa, pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali na Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news