Rais Dkt.Mwinyi ashiriki dhifa ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na Rais Dkt.Samia kwa Rais wa Namibia

DAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na Viongozi Wakuu wa Serikali katika Dhifa ya Chakula cha Usiku iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa heshima ya Rais wa Namibia, Mhe. Dkt. Netumbo Nandi-Ndaitwah.
Hafla hiyo imefanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei 2025.
Rais Dkt. Netumbo yupo nchini kwa ziara ya kikazi, ikiwa ni ziara yake ya kwanza kutembelea Tanzania tangu achaguliwe kuwa Rais wa Namibia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news