TCB yadhamiria kuendeleza mageuzi ya kidijitali,kuongeza ujumuishi wa kifedha

DAR-Benki ya Biashara ya Tanzania (TCB) imejipanga kuendeleza mageuzi ya kidijitali ili kuongeza ujumuishi wa kifedha kwa wajasiriamali wadogo na wa kati.
Katika upande wa ukuaji wa mizania ya kifedha,jumla ya mali za benki zimeongezeka kwa asilimia 25 hadi kufikia shilingi trilioni 1.74, na amana za wateja zimefikia shilingi trilioni 1.17 ikiwa ni ishara ya kuongezeka kwa imani ya wateja.
Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TCB, Martin Emmenuel Kilimba katika mkutano mkuu wa 33 wa wanahisa.

Amesema, benki hiyo inaweka mkazo kwenye kuboresha miundombinu ya teknolojia ya kidijitali na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa makundi hayo muhimu ya uchumi, kwa lengo la kuchochea maendeleo ya sekta binafsi na ukuaji wa uchumi kwa ujumla.

Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa 33 wa Wanahisa wa benki hiyo,Mkurugenzi Mtendaji wa TCB, Bw. Adam Mihayo amesema?TCB inalenga kuongeza ufanisi katika matumizi ya teknolojia mwaka huu wa fedha.

Vilevile kuendeleza suluhisho bora kwa wajasiriamali,kwani SMEs huchangia zaidi ya asilimia 95 ya biashara zote nchini na takribani asilimia 35 ya Pato la Taifa, hivyo kuwekeza katika huduma za kidijitali ni hatua muhimu ya kukuza sekta hiyo.

Bw. Mihayo amefafanua pia mafanikio ya kifedha yaliyopatikana mwaka 2024, ambapo benki ilipata faida kabla ya kodi ya shilingi bilioni 44.81, kutoka kwenye hasara ya shilingi bilioni 44.42 mwaka 2023.
Pia,amesema faida baada ya kodi ilipanda kwa asilimia 170 na kufikia shilingi bilioni 32.62, ikiwa ni matokeo ya ongezeko la mapato ya riba halisi na mapato mengine ya uendeshaji, huku gharama za riba zikibaki chini ya mapato yaliyopatikana.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news