TRC yatoa ufafanuzi ajali ya treni ya Mjini kwenda Pugu

DAR-Shirika la Reli Tanzania (TRC) limethibitisha kutokea kwa ajali ya treni ya mjini kwenda Pugu leo jioni majira ya saa 10:05, katika makutano ya reli na barabara ya Kawawa, ikiwa na mabehewa 12 yaliyojaa abiria takribani 1,200.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TRC, ajali hiyo ilisababisha majeruhi 10 wakiwemo wanaume wawili na wanawake wanane ambao walikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Amana kwa matibabu zaidi. Mabehewa sita kati ya 12 yalipata athari kutokana na ajali hiyo.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika na uchunguzi unaendelea. TRC imeahidi kutoa taarifa zaidi mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Huduma ya treni kati ya Stesheni ya Kamata na Pugu inatarajiwa kurejea kama kawaida kesho. TRC imetoa pole kwa wote walioathirika na ajali hiyo kwa namna moja au nyingine.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news