Wizara ya Ardhi yahamia jengo jipya Mji wa Serikali Mtumba

DODOMA-Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi leo Mei 19,2025 imehamia rasmi katika jengo lake jipya lililopo katika mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi pamoja na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhandisi Anthony Sanga waliwaongoza watumishi wa wizara hiyo kuhamia kwenye jengo hilo.
"Leo hii sisi tumehamia rasmi na tuko tayari kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi na wote wanaokuja katika ofisi zetu basi wakaribie hapa Mtumba kwa sababu sasa majukumu rasmi yatakuwa yakitolewa hapa," amesema Mhe. Ndejembi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news