Yustas Rwamugira wa TLP achaguliwa kuwania Urais 2025

DAR-Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) kimemchagua,Yustas Rwamugira kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba,mwaka huu.
Hatua hiyo imefikiwa katika Uchaguzi Mkuu wa chama hicho uliofanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi wa chama hicho Mei 26,2025 Mwenyekiti wa uchaguzi huo Coaster Jimmy, amesema jumla ya wapiga kura walikuwa 103.

Kati ya hizo Yustas Rwamugira ambaye ni Katibu Mkuu wa TLP amepata kura 51 huku washindani wenzake Neema Nyerere akipata kura sita,Wilson Ellas kura 46.

Yustas Rwamugira amewashukuru wanachama kwa kuonesha imani kubwa kwake huku akiahidi kuwa yeye na mgombea mweza wake, Amana Selemani Mzee watakiwakilisha vema chama hicho.

Msajili Msaidizi wa vyama vya Siasa Tanzania, Sisty Nyahoza amewapongeza Tanzania Labour Party TLP, kwa kufanya uchaguzi kwa amani wa chama hicho huku akiwatakia kila la heri.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news