Balozi CP Hamad ateta na Wawakilishi wa Diaspora nchini Msumbiji

MAPUTO-Juni 19,2025 Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji anayewakilisha mataifa ya Madagascar na Ufalme wa Eswatini,Mheshimiwa CP Hamad Khamis Hamad amekutana na Wawakilishi wa Diaspora waliopo Maputo kwenye Viwanja vya Ubalozi jijini Maputo.
Katika mkutano huo, mbali ya kupokea changamoto zinazowakabili Diaspora hao, aliwasisitiza kuwa raia na mabalozi wema kwa muda wote watakapokuwa Msumbiji.
Aidha, aliwahakikishia kwamba Ubalozi utatoa kila aina ya msaada na ushirikiano katika kutatua changamoto zao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news