BoT yazishika mkono taasisi za kijamii Mbeya ikiadhimisha miaka 59

MBEYA-Katika kuadhimisha miaka 59 tangu kuanzishwa kwa Benki Kuu ya Tanzania, Tawi la Benki Kuu Mbeya limetoa msaada wa vifaa na mahitaji mbalimbali kwa taasisi za kijamii katika mkoa huo.
Msaada huo umejumuisha viti 25 na meza 12 kwa Shule ya Msingi Itiji, mashuka 200, mashine moja ya kupima shinikizo la damu (BP machine), pamoja na viti vitatu vya magurudumu kwa Hospitali Teule Mbalizi.
Aidha, msaada wa chakula umetolewa kwa Kituo cha Watoto Yatima cha HOPE, ikiwa ni sehemu ya mchango wa benki katika kuunga mkono jamii inayoizunguka.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news