Derby ya Kariakoo kuchezeshwa na waamuzi kutoka Misri

DAR-Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imetangaza maofisa wa mchezo wa Dabi ya Kariakoo kwenye Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara kati ya wenyeji Young Africans SC dhidi ya Simba SC.

Taarifa ya bodi imebainisha kuwa, mchezo huo namba 184 utachezeshwa na waamuzi kutoka nchini Misri.

Pia, taarifa hiyo imebainisha kuwa,Mwamuzi wa kati atakuwa Amin Mohamed Amin Omar kutoka Misri akisaidiwa na Mahmoud Ahmed Abo El Regal kama Mwamuzi msaidizi namba moja na Samir Gamal Saad Mohamed ambaye atakuwa msaidizi namba mbili.

Aidha,Kamishna wa mchezo huo utakaopigwa Juni 25, 2025 saa 11:00 jioni katika dimba la Benjamin Mkapa anatarajiwa kuwa Salim Omary Singano.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news