Mama Mariam Mwinyi afanya mazungumzo na uongozi wa Multi Click Digital Solutions

ZANZIBAR-Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation(ZMBF), Mhe. Mama Mariam Mwinyi ameushukuru uongozi wa Multi Click Digital Solutions Ltd kwa utayari wao kushirikiana na ZMBF katika safari ya mageuzi ya kidijitali yenye tija kwa maendeleo.
Mama Mariam Mwinyi amesema hayo alipokutana na Uongozi wa Multi Click Digital Solutions Ltd katika Ofisi zake Migombani, Mkoa wa Mjini Magharibi leo Juni 5,2025.
Katika mazungumzo yao yalihusu kutumia teknolojia katika kuboresha ufanisi wa utoaji wa huduma bora kwa jami ikiwemo uanzishaji wa mifumo ya kidijitali kwa ajili ya utawala bora, usimamizi wa taarifa, na utoaji wa huduma rafiki kwa jamii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news