Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yateta na wakuu wa vitengo vya sheria halmashauri za Mwanza

MWANZA-Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mwanza, tarehe 10 Juni 2025 imekutana na kufanya kikao na wakuu wa vitengo vya sheria wa halmashauri za Mkoa wa Mwanza.Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mjini Mwanza na kimeongozwa na Wakili wa Serikali wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Kadyemela Lushagara

Lengo la kikao hicho ilikuwa ni kukutana na Wakuu wa Vitengo vya Sheria Mkoa wa Mwanza na kuwafahamisha juu ya uwepo wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika Mkoa wa Mwanza na huduma za kisheria zitolewazo na Ofisi hiyo.
Kikao hicho pia kimejadili na kuazimia namna bora ya Mawakili wa Serikali wa Halmashauri kutekeleza majukumu yao katika mwaka wa fedha ujao 2025/2026 hasa katika eneo la Uingiaji wa Mikataba, Usimamizi wa Miradi ya Uwekezaji na Maendeleo, Uendeshaji wa Kamati za Ushauri wa Kisheria za Wilaya, na

Ushiriki wao katika zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news