Serikali yatoa msimamo kuhusu Derby ya Kariakoo

DODOMA-Serikali imesema kuwa, inaendelea kufuatilia kwa makini sakata la mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na Simba, lakini haitangilia moja kwa moja kuepuka vikwazo vya FIFA huku ikisisitiza kanuni na sheria zilizowekwa za uendeshaji wa mpira zifuatwe.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma amesema hayo leo Juni 11 2025 Bungeni jijini Dodoma alipojibu swali la nyongeza la mbunge wa Makete, Mhe. Festo Sanga.

"Tunafuatilia kwa ukaribu namna mgogoro unavyoendelea kutatulia huku tukijaribu kwa kiwango kikubwa kutoingilia maamuzi ya TFF na bodi ya ligi na tunasisitiza mamalaka kufuata kanuni na sheria walizojiwekea za Mpira wa miguu,” amesema Mhe. Hamis Mwinjuma

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news