Ubingwa wa PSG kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya na Pyramids kwenye Ligi ya mabingwa Afrika ndio mapito ya Simba Sports Club

NA AHMED ALLY
Msemaji Simba SC

MWAKA 2011 PSG ilininunuliwa na Qatar Sports Investments kwa hisa za asilimia 87.5 baada ya hapo Tajiri amejaribu kutawala soka la Ulaya lakini hakufanikiwa

Safari yake imeenda sambamba na kusajili wachezaji wakubwa duniani kama Messi, Neymar na wengineo lakini bado hakufikia malengo

Miaka 14 baada ya uwekezaji wake ndio PSG imefanikiwa kubeba Ubingwa Ulaya.

Pyramdis ilinunuliwa na Tajiri kutoka Falme za kiarabu (UAE) Salem Al Shamsi mwaka 2019.

Baada ya Al Shamsi kuinunua Pyramids imemlazimu kusubiri kwa miaka sita kuchukua ubingwa wa Afrika

Njia ya Tajiri wa PSG na Pyramids ndio anayopitia tajiri wa Simba Sports,Mohamed Dewji (Mo Dewji).
Mo Dewji ameingia rasmi Simba mwaka 2018 akiwa Mwekezaji wa hisa 49, ndani ya miaka saba ya uwekezaji wake Simba imecheza Fainali ya Afrika.

Hii ni hatua kubwa sana kwa Simba na Mo Dewji kwenye malengo yao kutawala soka la Afrika.

Muhimu kwetu wana Simba ni kuwa na subira, ukubwa wa Afrika ndio kitu tunachokitafuta hivi sasa na hatupo mbali kufikia

Tumpe support mwekezaji wetu kama walivyofanya PSG na Pyramids na tuendelee kuinga mkono timu yetu bila kuchoka.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news