DAR-Waziri wa Uchukuzi wa Anga wa Jamhuri ya Somalia, Mhe Mohamed Nuh Juni 30, 2025 amefanya ziara katika Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania kuangazia fursa mbalimbali za ushirikiano wa kiuchumi katika sekta ya anga.

Kwa upande wake Bw. Msangi ameeleza kuwa TCAA inaendelea kupanua Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) na kusisitiza kuongeza nguvu katika kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi katika masomo ya anga.
Aidha, ameshukuru kwa idadi ya wanafunzi kutoka Somalia wanaochukua kozi chuoni hapo.
Katika hatua nyingine, Somalia imeeleza kuwa ni iko tayari kuboresha ushirikiano wa uwili na Tanzania katika Sekta ya Usafiri wa Anga.