Bodi ya Ligi Kuu yaipiga faini Simba SC

DAR-Klabu ya Simba SC imetozwa faini ya shilingi milioni tatu kwa makosa matatu waliyoyafanya katika mchezo namba 184 wa Derby ya Kariakoo dhidi ya Yanga SC uliomalizika kwa Yanga Sc kushinda 2-0 katika dimba la Benjamin Mkapa mnamo Juni 25, 2025 jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya Julai 17, 2025 ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Simba SC imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya shilingi milioni moja kwa kosa la kushindwa kuhudhuria mkutano wa wanahabari uliofanyika kwenye ukumbi wa Benki ya Taifa ya Biashara Dar es Salaam Juni 24, 2025 kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:58 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Katika hatua nyingine kikao cha Kamati ya TPLB kilichofanyika Julai 15, 2025 kimetoa uamuzi wa kuiadhibu Simba SC kwa kuitoza faini ya shilingi milioni moja kwa kosa la kushindwa kuhudhuria kikao cha kitaalam cha maandalizi ya mchezo (MCM) Juni 24, 2025 kinyume na matakwa ya Kanuni ya 17:2(2.2) ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Pia,Simba SC imeadhibiwa kwa kutozwa faini ya milioni moja kwa kosa la kuingia kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kupitia mlango usio rasmi kuelekea mchezo huo uliochezwa Juni 25, 2025.

Hiyo ikiwa ni kinyume na matakwa ya kanuni ya 17:21 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo, adhabu ambazo zimetolewa kwa mujibu wa kanuni ya 17:62 ya Ligi Kuu kuhusu Taratibu za Mchezo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news