Chuo Kikuu Mzumbe kuweka Kambi Maalumu za Udahili kwa mwaka wa masomo

MOROGORO-Chuo Kikuu Mzumbe kinapenda kuwataarifu Wanafunzi, wazazi na Wadau wa elimu kitakuwa na Kambi Maalumu za Udahili kwa mwaka wa masomo 2025/2026 kuanzia tarehe 13 hadi 22 Julai 2025, katika mikoa ifuatayo;

Dar es Salaam - Mlimani City Mall

Mwanza – Rock City Mall

Dodoma – Viwanja vya Nyerere Square

Arusha – Uwanja wa Makumbusho

Mbeya - Stendi ya Kabwe

Huduma zitakazotolewa ni Pamoja na; Elimu ya uchaguzi wa kozi na vigezo vya kujiunga, Ushauri wa kitaaluma kwa wanafunzi watarajiwa (Career guidance),huduma ya udahili wa papo kwa hapo.
Hii ni nafasi ya kipekee kwa wazazi, wanafunzi na wadau wa elimu kufika na kupata huduma za moja kwa moja katika msimu huu wa dirisha la udahili kwa Wanafunzi wa elimu ya juu kutoka kwa Maafisa mahiri wa Chuo Kikuu Mzumbe.

Huduma zitatolewa kila siku kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.Hakuna kiingilio na ushauri unatolewa bila malipo.

Wadau wote mnakaribishwa.Kwa taarifa zaidi, tafadhali tufuatilie katika mitandao yetu ya kijamii na tovuti ya Chuo Kikuu Cha Mzumbe.

Karibu Chuo Kikuu Mzumbe, “Tujifunze kwa Maendeleo ya Watu”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news