Heko kidato cha sita


Utenzi wa pongezi kwa wahitimu wa kidato cha Sita wa mwaka 2025 ambao matokeo ya mitihani yao yametangazwa tarehe 06 Julai, 2025 na Baraza la Mitihani la Tanzania.

¹Pongezi kwenu cha Sita
Matokeo kuyapata
Masomo 'liyafumbata
Mmefaulu kishindo

²Hakika mlijikita
Masomo kuyachakata
Leo hii metakata
Ufaulu wa kishindo

³Masomo mlikamata
Juhudi mkazingata
Hakika mmekung'uta
Ufaulu maridhawa

⁴Pokeni zetu pongezi
Kwa nzurisa' yenu kazi
Hamkufanya ajizi
Mmetisha kwa kishindo

⁵Pongezi pia wazazi
Jamii wote walezi
Ni wao wema ulezi
Mmeshinda kwa kishindo

⁶Heko kwao viongozi
Kwa shule usimamizi
Na walimu chapakazi
Cha Sita mmetusua

⁷Sasa muipande ngazi
Ya maarifa ujuzi
Pamoja na ubobezi
Chuo Kikuu Huria

⁸Huria cha Tanzania
Pongezi chawapatia
Na heko twairudia
Kongoleni wahitimu

MTUNZI
Dkt. Mohamed Maguo
Mhadhiri Mwandamizi
Mkuu wa Itifaki
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news