Magazeti leo Julai 18,2025

WARATIBU wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) katika mikoa ya Lindi na Mtwara wametakiwa kutojihusisha na makundi mbalimbali ya Whatsapp kipindi hiki wanapoelekea katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba,2025.
Hayo yamejiri Julai 17 wakati wa kufunga mafunzo ya siku tatu kwa waratibu hao yaliyofanyika kwenye Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara.

Akizungumza kwa niaba ya Mjumbe wa INEC, Mratibu wa Mafunzo wa INEC, Cecilia Sapanjo amesema katika kipindi hicho cha mchakato huo wa uchaguzi wasijihusishe kutuma taarifa yoyote kwenye makundi hayo kwani kufanya hivyo ni kutenda kosa chini ya sheria na watawajibika kwa kosa hilo.

"Hivi sasa yapo magrupu mengi ya Whatsapp jitahidini katika kipindi hiki tuyapunguze ili tusije kukosea tukatuma taarifa yoyote katika magrupu haya,"amesisitiza Cecilia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news