Magazeti leo Julai 19,2025

WANAFUNZI wawili wa kidato cha nne wa Shule ya Morogoro Sekondari, Lusajo Mwang’onda (18) na Ghalib Omary (18) wakazi wa Kata ya Kihonda Maghorofani , Manispaa ya Morogoro wamefariki dunia kutokana na ajali ya bodaboda iliyowabeba kwenda shule kuparamia lori barabara kuu ya Morogoro- Dodoma.
Dereva wa bodaboda hiyo, Baraka Sijawaza Sajio (22) pia mkazi wa Kihonda Maghorofani, naye alifariki dunia papo hapo kwenye ajali hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Alex Mkama amesema ajali hiyo imetokea Julai 18,2025 saa moja asubuhi eneo la Samaki Samaki Bima

Amesema, pikipiki yenye namba za usajili MC.534 DYX, ikiendeshwa na Sajio ikitokea Kihonda kwenda Morogoro mjini, ikiwa imewabeba abiria wawili iligongana na gari lenye namba za usajili T .310 DQC lenye tela T.646 ANQ likiendeshwa na Simba Omary Juma, (45) mkazi wa Tandale jijini Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news