Magazeti leo Julai 26,2025

ENEO la hifadhi ya Ngorongoro limeendelea kuwa kimbilio la wageni mashuhuri duniani ambapo siku ya leo, Meya wa Jiji la Dallas nchini Marekani, Mhe. Eric Johnson kwa mara ya kwanza ameshuhudia upekee wa vivutio vya utalii vilivyopo katika hifadhi hiyo.
Meya huyo aliyefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Dkt. Elsie Kanza amepokelewa na Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA), Abdul-Razaq Badru na kuwaeleza kuwa eneo la hifadhi ya Ngorongoro lina utajiri wa vivutio vya utalii ikiwepo Kreta ya Ngorongoro, Wanyama wakubwa watano "Big Five", bonde la Olduvai lenye gunduzi mbalimbali za Zamadam, tambarare za Ndutu ambazo ni mazalia ya Nyumbu, mchanga unaohama, Nyayo za Laetoli zenye umri wa miaka milioni 3.7 iliyopita na vivutio vingine vingi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news