Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiongozwa na Mwenyekiti wake Dkt. Samia Suluhu Hassan, kimepitisha kwa kishindo marekebisho ya Katiba yake ya mwaka 1977 (toleo la Mei 2025), baada ya kura ya maoni ya ndani ya chama kuonyesha uungwaji mkono wa asilimia 99.8 kutoka kwa wajumbe wa Mkutano Maalum wa CCM uliofanyika Jumamosi kwa njia ya mtandao.
Matokeo ya kura hiyo yalitangazwa rasmi na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Idara ya Oganaizesheni, Issa Haji Ussi Gavu, aliyesema kuwa jumla ya wajumbe 1,915 walishiriki katika upigaji kura, kati ya wajumbe 1,931 waliotarajiwa.
“Idadi ya wajumbe, jumla ya wajumbe wote ambao wanatakiwa kupiga kura hii ni 1931 kama ambavyo tulitangaziwa hapo awali, lakini wajumbe waliohudhuria ni 1915, wajumbe wasiohudhuria ni wajumbe 16, wajumbe waliopiga kura ni wajumbe 1915 lakini kura za hapana ni sifuri, kura zilizoharibika ni tatu, kura za ndiyo ni 1912 hiyo ni sawa na asilimia 99.8.”
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo













